.BAADA YA MUHONG KUJIUZULU ZITTO KABWE YAMPONGOZA

1 ·
Nimepata taarifa kuwa Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini Ndugu Sospeter Muhongo amechukuwa hatua ya kujiuzulu katika nafasi hiyo. Napenda kuchukua nafasi hii kutambua busara aliyochukua ambayo naamini itasaidia harakati za kujenga demokrasia yenye uwajibikaji. Naamini uamuzi wa Ndugu Muhongo umewezesha kulinda heshima ya Bunge na maazimio yake. Kwa muda mfupi alioongoza Wizara hiyo, Ndugu Muhongo ameweza kuongoza mabadiliko kadhaa muhimu ya kiutendaji katika wizara hiyo na taasisi zake. Hata hivyo, nafasi ya Wizara aliyokuwa anaongoza katika suala la Tegeta Escrow imemtia doa kubwa ambalo ilikuwa lazima awajibike. Naamini Rais Kikwete atamteua mtu mchapakazi na makini zaidi atakayeweza kuendeleza yale mazuri ya Ndugu Muhongo na kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza.

TOA MAONI YAKO HAPA

JIUNGE NASI KWA KU LIKE PAGE YETU HAPA CHINI


EmoticonEmoticon