MWENYEKITI WA CHADEMA JIMBO LA UKONGA ATANGAZA KUJIUZULU PAMOJA WAJUMBE WOTE

BW  THOMAS  NYAHENDE  AMBAYE  ALIKUWA  NI  MWENYEKITI   WA  JIMBO  LA  UKONGE

KAULI  YAKE  KUPITIA  UKARASA  WAKE  WA  FACEBOOK
· 
Makamanda na Marafiki zangu wote,
Napenda kuwafahamisha kuwa Jana Jumamosi tarehe 24 January 2015 nimetangaza rasmi kujiuzulu nafasi yangu ya Mwenyekiti Jimbo la UKONGA. Katika hali hiyo wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji Jimbo la UKONGA nao wamejiuzulu ili kuungana na Mwenyekiti wao.
Hatua hiyo ngumu sana tumeifikia jana baada ya kushauriana na Mwenyekiti wetu wa Taifa Kamanda Mbowe kufuatia hali ya sintofahamu iliyokuwepo kwa muda mrefu baina ya Viongozi wa Jimbo la UKONGA na Mratibu wa Kanda yetu ya Pwani. Tumefikia uamuzi huo kwa ajili ya kuzingatia maslahi mapana ya CHADEMA Jimbo la UKONGA.
Nawashukuru sana makamanda na marafiki wote ambao mmekuwa mkiniunga mkono katika utekelezaji wa majukumu yangu nikiwa Mwenyekiti wa Jimbo la UKONGA. Sasa niwaombe tuendelee kuisupport CHADEMA na hasa Uongozi wa Mpito utakaoundwa hivi karibuni wakati taratibu za kuitisha uchaguzi mpya zikiandaliwa.
Sasa tujielekeze katika kuijenga upya kanda yetu ya Pwani iliyokuwa imedorora, ili iweze kutuunganisha na kuratibu shughuli za chama katika kanda yetu na hatimaye kanda yetu iweze kuwa kitovu na kiongozi wa mabadiliko ya uongozi katika nchi hii tunapofanya uchaguzi mkuu baadae mwaka huu 2015.
ALUTA CONTINUA...MAPAMBANO BADO YANAENDELEA

TOA MAONI YAKO HAPA

JIUNGE NASI KWA KU LIKE PAGE YETU HAPA CHINI


EmoticonEmoticon